16 February 2016

List kamili ya washindi tuzo za Grammy, na rekodi ya Rapa Kendrick Lamar.


Tuzo za muziki nchini Marekani na kubwa Duniani, Grammy, zimefanyika jana Febr 15 mjini Los Angels huku tukishuhudia wakali kadhaa wakiibuka na tuzo hizo akiwemo rapa kutoka Compton Kendrick Lamar aliyezibeba tuzo 5.
Ameongoza kwa kushinda tuzo 5 kwenye Tuzo za Grammy mwaka huu (58th Grammys) Lamar alikuwa amependekezwa vipengele 11 na kuweka historia ya kuongoza na nominations mwaka huu.
Msanii aliyewai kuweka rekodi hiyo ni King of Pop, Michael Jackson mwaka 1984 ambapo MJ alishinda tuzo 8 kati ya nominations 12.
Na bado haijavunjwa. Bado kendrick anapata heshima kubwa ya kuwa nominated mara 11 na kushinda tuzo 5 usiku mmoja.
KENDRICK alishinda 1. Best Rap Performance (“Alright”), 2. Best Rap/Sung Collaboration (“These Walls,” with Bilal, Anna Wise and Thundercat), 3. Best Rap Song (“Alright”), 4. Best Music Video (“Bad Blood,” withTaylor Swift) na 5. Best Rap Album.
Tazama list kamili ya washindi hapo chini,
RECORD OF THE YEAR
“Really Love” – D’Angelo And The Vanguard
“Uptown Funk” – Mark Ronson Featuring Bruno Mars
“Thinking Out Loud” – Ed Sheeran
“Blank Space” – Taylor Swift
“Can’t Feel My Face” – The Weeknd
ALBUM OF THE YEAR
Sound & Color – Alabama Shakes
To Pimp A Butterfly – Kendrick Lamar
Traveller – Chris Stapleton
1989 – Taylor Swift
Beauty Behind The Madness – The Weeknd
BEST NEW ARTIST
Courtney Barnett
James Bay
Sam Hunt
Tori Kelly
Meghan Trainor
SONG OF THE YEAR
“Alright” – Kendrick Lamar
“Blank Space” – Taylor Swift
“Girl Crush” – Little Big Town
“See You Again” – Wiz Khalifa Featuring Charlie Puth
“Thinking Out Loud” – Ed Sheeran
BEST POP SOLO PERFORMANCE
“Heartbeat Song” – Kelly Clarkson
“Love Me Like You Do” – Ellie Goulding
“Thinking Out Loud” – Ed Sheeran
“Blank Space” – Taylor Swift
“Can’t Feel My Face” – The Weeknd
BEST POP DUO/GROUP PERFORMANCE
“Ship To Wreck” – Florence + The Machine
“Sugar” – Maroon 5
“Uptown Funk” – Mark Ronson Featuring Bruno Mars
“Bad Blood” – Taylor Swift Featuring Kendrick Lamar
“See You Again” – Wiz Khalifa Featuring Charlie Puth
BEST POP VOCAL ALBUM
Piece By Piece – Kelly Clarkson
How Big, How Blue, How Beautiful – Florence + The Machine
Uptown Special – Mark Ronson
1989 – Taylor Swift
Before This World – James Taylor
BEST DANCE RECORDING
“We’re All We Need” – Above & Beyond Featuring Zoë Johnston
“Go” – The Chemical Brothers
“Never Catch Me” – Flying Lotus Featuring Kendrick Lamar
“Runaway (U & I)” – Galantis
“Where Are Ü Now” – Skrillex And Diplo With Justin Bieber
BEST DANCE/ELECTRONIC ALBUM
Our Love – Caribou
Born In The Echoes – The Chemical Brothers
Caracal – Disclosure
In Colour – Jamie XX
Skrillex And Diplo Present Jack Ü – Skrillex And Diplo
BEST R&B PERFORMANCE
“If I Don’t Have You” – Tamar Braxton
“Rise Up” – Andra Day
“Breathing Underwater” – Hiatus Kaiyote
“Planes” – Jeremih Featuring J. Cole
“Earned It (Fifty Shades Of Grey)” – The Weeknd
BEST TRADITIONAL R&B PERFORMANCE
“He Is” – Faith Evans
“Little Ghetto Boy” – Lalah Hathaway
“Let It Burn” – Jazmine Sullivan
“Shame” – Tyrese
“My Favorite Part Of You” – Charlie Wilson
BEST R&B SONG
“Coffee” – Miguel
“Earned It” – The Weeknd
“Let It Burn” – Jazmine Sullivan
“Really Love” – D’Angelo And The Vanguard
“Shame” – Tyrese
BEST URBAN CONTEMPORARY ALBUM
Ego Death – The Internet
You Should Be Here – Kehlani
Blood – Lianne La Havas
Wildheart – Miguel
Beauty Behind The Madness – The Weeknd
BEST R&B ALBUM
Coming Home – Leon Bridges
Black Messiah – D’Angelo And The Vanguard
Cheers To The Fall – Andra Day
Reality Show – Jazmine Sullivan
Forever Charlie – Charlie Wilson
BEST RAP PERFORMANCE
“Apparently” – J. Cole
“Back To Back” – Drake
“Trap Queen” – Fetty Wap
“Alright” – Kendrick Lamar
“Truffle Butter” – Nicki Minaj Featuring Drake & Lil Wayne
“All Day” – Kanye West Featuring Theophilus London, Allan Kingdom & Paul McCartney
BEST RAP/SUNG COLLABORATION
“One Man Can Change The World” – Big Sean Featuring Kanye West & John Legend
“Glory” – Common & John Legend
“Classic Man” – Jidenna Featuring Roman GianArthur
“These Walls” – Kendrick Lamar Featuring Bilal, Anna Wise & Thundercat
“Only” – Nicki Minaj Featuring Drake, Lil Wayne & Chris Brown
BEST RAP SONG
“All Day” – Kanye West Featuring Theophilus London, Allan Kingdom & Paul McCartney
“Alright” – Kendrick Lamar
“Energy” – Drake
“Glory” – Common & John Legend
“Trap Queen” – Fetty Wap
BEST RAP ALBUM
2014 Forest Hills Drive – J. Cole
Compton – Dr. Dre
If You’re Reading This It’s Too Late – Drake
To Pimp A Butterfly – Kendrick Lamar
The Pinkprint – Nicki Minaj
BEST COMPILATION SOUNDTRACK FOR VISUAL MEDIA
Empire: Season 1 – Various Artists
Fifty Shades Of Grey – Various Artists
Glen Campbell: I’ll Be Me – Various Artists
Pitch Perfect 2 – Various Artists
Selma – Various Artists
BEST SONG WRITTEN FOR VISUAL MEDIA
“Earned It” – The Weeknd
“Glory” – Common & John Legend
“Love Me Like You Do” – Ellie Goulding
“See You Again” – Wiz Khalifa Featuring Charlie Puth
“Til It Happens To You” – Lady Gaga
PRODUCER OF THE YEAR, NON-CLASSICAL
Jeff Bhasker
Dave Cobb
Diplo
Larry Klein
Blake Mills
BEST MUSIC VIDEO
“LSD” – ASAP Rocky
“I Feel Love (Every Million Miles)” – The Dead Weather
“Alright” – Kendrick Lamar
“Bad Blood” – Taylor Swift Featuring Kendrick Lamar
“Freedom” – Pharrell Williams
BEST MUSIC FILM
Mr. Dynamite: The Rise Of James Brown
Sonic Highways
What Happened, Miss Simone?
The Wall
Amy

BREAKING NEWZZ......MSANII WA BONGO FLAVOUR Joni Woka afariki dunia

Akiongea kwa simu kaka wa marehemu Omari Milay, amesema walipigiwa simu alfajiri ya leo na kujulishwa kuwa Joni Woka amefariki katika hospitali ya Muhimbili, alipokuwa akipata matibabu ya ajali aliyopata siku ya jana.
Joni Woka alipata ajali ya kugongwa na kitu kizito kwenye paji la uso, alipokuwa garage maeneo ya Sinza akitengeneza gari yake, kwa bahati mbaya mtungi wa gesi ukalipuka na moja ya vipande vya chuma chenye ncha kali kikamchoma kichwani,
Tarifa za awali za madaktari zilisema wanahofia kipande hiko kimefika mbali kiasi kwamba damu inamwagikia kwenye ubongo.
Mipango ya mazishi familia imesema inakutana kujadili na mara itakapokamilika watajulisha watu nini kinaendelea.
Msanii John Woka ambaye alikuwa kwenye kundi la Watukutu Family, alijipatia umaarufu kwa nyimbo zake za Sophia, baby gal na nyinginezo, ambazo aliziimba kwa mtindo wa ulevi.

15 February 2016

Ndege ya Air Tanzania Yanusurika Kuwaka Moto Katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere

Msemo wa waswahili kwamba ng’ombe wa maskini hazai unaonekana kuwa kweli kwa Shirika la Ndege Nchini (ATCL), ambalo ndege yake pekee imenusurika kuwaka moto katika uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam juzi.

Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa wakisafiri kwenda mataifa mbalimbali ambao walizungumza na Nipashe juzi jioni, ndege hiyo ilionekana ikitoa moshi mwingi hali iliyosababisha magari ya zimamoto kufika eno hilo ili kuzima moto.

Msafiri mmoja ambaye alikuwa akipanda ndege kuelekea Nairobi, Kenya aliliambia gazeti hili kuwa waliona ndege hiyo ya ATCL ikitoa moshi mwingi hali iliyoashiria kuwa kulikuwa na hitilafu kwenye injini yake.

“Tuko hapa na tunaiona ndege inatoa moshi kweli kweli, watafuteni wahusika wawaambie tatizo nini,” alisema abiria huyo ambaye baadaye alituma picha mbalimbali za mnato na video kwa njia ya simu zikionyesha ndege hiyo ikitoa moshi mwingi.

Gazeti hili liliwasiliana na Katibu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini, Ramadhani Maleta, ambaye alisema hawezi kulizungumzia suala hilo na alielekeza watafutwe wahusika wakuu ambao ni ATCL.

“Mimi siyajui hayo na wala siwezi kuwasemea wakati wenyewe wapo, watafuteni ATCL wao ndiyo wanauwezo wa kulizungumzia kwa kina suala hili, mimi kwanza siko kazini muda mrefu,” alisema Maleta.

Alipoulizwa kuhusu hitilafu ya ndege h iyo, Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga, TCAA, Bestina Magutu, aliliambia gazeti hili kuwa ni vyema suala hilo wakaulizwa wahusika ambao ni ATCL kwa kuwa yeye si msamaji wa shirika hilo.

Jitihada za kumpata msemaji wa ATCL hazikuzaa matunda jana.

Akizungumza wakati wa siku ya sheria nchini, Rais John Magufuli alielezea kushangazwa kwake na kudumaa kwa ATCL hata kushindwa kumudu kuwa na ndege zake kama yalivyo mashirika mengine ya ndege Afrika na duniani.

Rais Magufuli alisema ana uwezo wa kununua hadi ndege sita mpya za kuliendesha shirika hilo lakini lazima wapatikane watumishi ambao watakuwa na uwezo wa kuliendesha na ikiwezekana "kuwafuta wafanyakazi wote walioko sasa."

Source:Nipashe

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 15/2/2016


14 February 2016

Mwanamke, kumchuna mumeo ni sawa na kujiibia mwenyewe



Naongea hivi maana wanawake wengi wa leo tunashindwa kutofautisha mume na mtu mpita njia au kwa maneno mengine mtu usie na uhakika nae kwamba mtaishi wote kama mume na mke.

Unakuta mwanamke keshaolewa badala ya kumshauri mume wake wajenge future yao ya baadaye na watoto wao, eye ndo kwanza yuko busy anataka wigi la laki sita, anataka viatu vya laki 3, anataka Iphone, nguo za Woolworth, starehe kwa sana na kushughulikia vya tumbo tu anasahau wako kwa nyumba ya kupanga wala hana habari.

Simaanishi kwamba wanawake waume zenu wasiwapendezeshe but acheni kudemand vitu visivyo na tija badala ya kujenga future yenu. Mambo ya kucompete na mashost zako so nawe unataka uonekane umo unamgeuza mumeo buzi wakati ni mume wacha.

Mwanamke bana matumizi vizuri, weka mahesabu yako sawasawa, mshauri mumeo mfanye mambo ya maana achana na mawigi ya laki 6, kufanya showoff wakati hamna nyumba maana kesho watoto hawatalala kwenye hilo wigi la laki 6.

Umeshaolewa maana yake mko na huyo mumeo kujenga kesho yenu itayokuwa the best.
Wachaneni na vitu visivyo na maana pindi mkishaolewa, msaidie mumeo kujenga future yenu na sio kumchuna maana ni sawa na unajiibia mwenyewe

HAYA NDO MAJESHI 10 HATARI ZAIDI DUNIANI




                                                                Wanajeshi wa Korea Kusini wakifanya mazoezi. 
.

                                                                                                Wanajeshi wa Uturuki.
.

                                                                                                     Wanajeshi wa Ujerumani.

0.

                                                                                          Wanajeshi wa Ufaransa. 


                                                                                         Waajeshi wa Uingereza.
.

                                                                Wananchi wa India wakiwa katika mazoezi.

                                                                                                        Wanajeshi wa China.


                                                                                                             Wanajeshi wa Urusi.

                                                                                                                      MAREKANI.

Nimegundua Mimi na Baba Yangu Mzazi Tunashare Msichana Mmoja Bila Kujua...

Ni wiki ya tatu sasa tangu mama asafiri kwenda kwenye msiba huko nyumbani kwao, nyumbani tumebaki mimi, baba na mfanyakazi wetu wa ndani.
Kwa vile mimi nimeshamaliza chuo na muda mwingi huwa nashinda nyumbani (sina kazi) nimejikuta nikiingia katika mahusiano ya mapenzi na huyu msichana waa kazi.
Juzi usiku kama kawaidayangu nilienda chumbani kwake ila sikumkuta ikabidi nitege mingo ili nijue huyu msichana kaenda wapi, baada ya kama lisaa 1 nilishtuka kuona mlango wa kwa baba unafunguliwa na yule msichana wa kazi kakatoka na kwenda chumbani kwake.
Niliumia sana kuona kile kitendo si kwa wivu wa mapenzi bali kwa kile kitendo alichofanya baba na ukizingatia anamke wa ndoa (mama yangu).
Wadau naombeni busara zenu kuwa anachokifanya sio kizuri au nimwambie na bi mkubwa?

HIVI NDIVYO DIAMOND ALIVYO POKELEWA NA UMATI MKUBWA WA WATU MJINI TURKANA NCHINI KENYA

Outside the airport!!....Nje ya Airport ya TURKANA LODWAR KENYA wakati tunatoka na njiani

Official VIDEO | Darassa Ft. Rich Mavoko - Kama Utanipenda

Mfanyakazi wa Tanesco wilayani kilosa apata kichapo kutoka kwa wananchi.

Wananchi wa kijiji cha Lumuma wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro wameandamana kwa kufunga barabara na kumpiga mfanyakazi wa shirika la ugavi wa umeme Tanesco wakilalamikia shirika hilo kupitisha nguzo za umeme kwenye mashamba yao kupeleka nishati hiyo katika vijiji jirani bila wao kupatiwa huduma hiyo.
Wakizungumza kijijini hapo wananchi hao wamesema wameamua kuandamana na kufunga barabara kufuataia shirika la umeme Tanesco kushindwa kusambaza huduma hiyo katika kijiji hicho na badala yake kupitisha nguzo katika maeneo yao kupeleka huduma katika vijiji vya jirani ambapo wamesema hawapotayari kuruhusu mradi huo kuendelea hadi watakapohakikishiwa kuunganishiwa nishati hiyo. 
 
Nao viongogozi wa kata na kijiji cha Lumuma wamesema wanaunga mkono wananchi kwani wamesema inaonekana zoezi hilo limegubikwa  na hujuma huku wameomba serikali na uongozi wa Tanesco kuona uwezekano wa kuanza kusambaza umeme katika kijiji cha Lumuma na badaye kumalizia katika vijiji vilivyoko katika kata hiyo.
 
Akiongea na ITV kwa  njia ya simu meneja Tanesco mkoa wa Morogpro Mhandisi John Bandiye amesema anatambua kuwepo mradi wa umeme katika kata ya Lumemo lakini hafahamu kama wananchi wa kijiji hicho wanalalamika na kwamba atafuatilia ili kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo.

Rais Magufuli awahamisha watumishi wa afya katika jengo la muhimbili, ili kina mama wanao lala chini waweze kutumia jengo hilo

 http://www.jamiiforums.com/attachments/12494926_463189047203881_5125711074879422530_n-jpg.323207/http://www.jamiiforums.com/attachments/12744572_463189043870548_8425244640278726175_n-jpg.323208/

Agizo la Rais Magufuli kuwataka watumishi wa Muhimbili kuhama ofisi ndani ya siku mbili ili kuwaachia majengo wagonjwa waliokosa nafasi hospitalini hapo laanza kutekelezwa.

Rais alitoa agizo hilo alipoenda kumjulia hali Mufti mkuu wa Waislamu Tanzania, sheikh Abubakari Zuberi aliyelazwa hospitalini hapo na kukuta mazingira ya wagonjwa wa wodi ya wazazi yakiwa hayaridhishi, ambapo alikutana na malalamiko ya wakina mama waliomfuata na kumueleza kuwa wamekuwa wakilazwa hadi watano kitanda kimoja huku mazingira yakiwa machafu kutokana na maji kuchuruzika kutoka maliwatoni.

Ofisi hizo zilizokuwa zikitumika na watumishi wa wizara ya afya sasa imeagizwa zirejeshwe chini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili walau kupunguza tatizo

RAIS MAGUFULI AMFANYA KINGUNGE KUVUNJA AHADI YAKE...NAKUTOA KAULI HII



Utendaji wa Rais John Magufuli baada ya siku 100 tangu alipoanza rasmi kazi kama kiongozi wa ngazi ya juu zaidi nchini, umezua mijadala mingi huku asilimia kubwa wakimpongeza kwa kazi nzuri lakini wengine wamesimama na yao.
Muendelezo wa kuchukua maoni ya wanasiasa wakongwe, wadau wa maendeleo na wananchi wa kawaida umegonga mwamba kwa mwanasiasa mkongwe, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru na kupelekea kuivunja ahadi yake aliyoitoa awali kuwa angempima Rais Magufuli baada ya siku 100.
Kingunge ambaye alitangaza kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuiweka kando kadi yake namba 8 baada ya kukitumikia chama hicho kwa zaidi ya miaka 60, na kumpigia debe Edward Lowassa (Chadema), amekataa kuikamilisha ahadi yake ya kuuzungumzia utendaji wa Magufuli huku akieleza kuwa hakuna mtu wa kumlazimisha kuitimiza ahadi hiyo.
“Hata kama niliahidi kuzungumza baada ya siku 100 lakini hakuna mwenye uwezo wa kunilazimisha kuzungumza,” Kingunge anakaririwa na gazeti la Nipashe. “Sitazungumza, waulizeni wengine watasema lakini mimi naomba mniache,” aliseongeza.
Kingunge alitangaza kujeungua CCM kwa madai kuwa chama hicho kimevunja katiba wakati wa mchakato wa kumpata mgombea wake wa urais na kwamba imepoteza dira kwa kuacha misingi ya uasisi wake

BREAKING NEWZZZ.....MBUNGE WA ZAMANI EZEKIEL WENJE APATA AJALI


Gari lililokuwa likiendeshwa na aliyekuwa Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje limepata ajali maeneo ya Magereza Bariadi mkoani Simiyu mchaba wa leo baada ya kuacha njia na kugonga mtaro na kisha kuanguka. Ndani ya gari hilo alikuwepo pia Mbunge wa VIti Maalumu (Chadema), Gimbi Masaba na Mwandishi wa habati wa Tanzania Daima, Sitta Tuma ambao wamepata michubuko kidogo.

KUWEPO KWA Askofu Gwajima Kwenye Mkutano wa Rais Magufuli na Wazee wa Dar es Salaam hiyo jana


Uwepo wa Askofu Gwajima kwenye mkutano wa Rais Magufuli na Wazee wa Dar es Salaam jana umepokelewa kwa hisia tofauti.

MGOMBEA URAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP ATUMIA ALAMA ZA CHADEMA KATIKA KAMPENI ZAKE

MGOMBEA URAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP ATUMIA ALAMA KAMA ZA CHADEMA KATIKA KAMPENI ZAKE..DONALT HUONYESHA ALAMA YA VIDOLE VIWILI JUU KAMA ILIVYO KUWA  CHAMA CHA CHADEMA KINAVYO TUMIA ALAMA HIYO KAMA INSHARA YA KUWATAMBULISHA.

HATIMAYE MKUU WA WILAYA YA KINONDONI PAUL MAKONDA AAMUA KUPANDA BODABODA

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI PAUL MAKONDA AKIWA KAPANDA KWENYE BODABODA AKIELEKEA KWENYE SHUGHULI ZAKE ZA KILA SIKU

Kauli ya Diamond Platnumz yamfanya Mrisho Mpoto asitishe kuachilia video ya 'Sizonje

Kauli ya staa wa muziki Diamond Platnumz ‘Kuna kushoot video na kurekodiwa’ imemfanya msanii wa muziki wa asili Mrisho Mpoto kuitia kapuni kwanza video yake mpya ya wimbo ‘Sizonje’ ili aichunguze kwanza kama inafaa.

Kupitia ukurasa wa instagram, Mpoto ameandika "Diamondplatnumz post yako ya leo imenifanya nisile Siku nzima. Nikiitafakari na sasa nimeamua kusitisha kutoa video yangu mpya ya #SIZONJE maana sina uhakika kama nime shoot au nimerecord. Ukimkimbiza sana mjusi anageuka kuwa nyoka"

Ijumaa hii Diamond aliachia video mpya ya wimbo ‘Make Me Sing’ akiwa na AKA wa Africa kusini na kutwitter.

Video: Pipi – Hello (Adele Cover)

---->ZAWADI NONO YA TSH. 30,000 TABIRI NANI ATAIBUKA MSHINDI LEO KATI YA..... (ARSENAL V/S LEICESTER CITY )





-TAJA NA IDADI YA MAGOLI.
-MSHINDI ATATANGAZWA HAPAHAPA
-COMMENT ZOTE ZIWE HAPO CHINI KWENYE FACEBOOK COMMENT BOX

SERIES: The Flash Season 2 Episode 13 | Download Link

The Flash Season 2 Episode 13! Download and Enjoy!!!!
 

Comments system

Disqus Shortname